Lissu akamwatwa na jeshi la Polisi Mbinga
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu amekamatwa na Jeshi la Polisi Wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma ambapo amekamatwa wakati alipomaliza mkutano wa hadhara uliofanyika leo April 09, 2025 katika Jimbo la Mbinga na taarifa iliyotolewa na CHADEMA imesema mpaka sasa haijulikani Lissu amepelekwa kituo gani cha Polisi.
Lissu amekamatwa pamoja na Wanachama wengine akiwemo Aden Mayala , Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kusini, Felius Festo , Mratibu wa Uhamasishaji BAVICHA Taifa, Shija Shebeshi na Mlinzi ambapo CHADEMA imelitaka Jeshi la Polisi kuwaachia Viongozi hao haraka na bila masharti yoyote.
CHADEMA imesema wakati wa zoezi la kumkamata Lissu, Wananchi wametawanywa kwa mabomu uwanjani na Polisi wametumia pia risasi za moto na kupelekea baadhi ya Wananchi kuumizwa. (video imerekodiwa muda mfupi kabla ya Lissu kukamatwa).
Jitihada za kulitafuta Jeshi la Polisi Mkoani Ruvuma ili kupata taarifa zaidi zinaendelea.
No comments:
Post a Comment