Wednesday, October 16, 2024

 Kamanda wa Polisi Jamii Wilaya ya Kipolisi Ukonga ASP Novatus Edmund Mallya amewaasa Polisi Jamii kuacha kutumia vibaya mwamvuli huo katika kutekeleza majukumu yao pamoja na ndani ya jamii wanayoishi.



ASP Mallya ameyasema hayo wakati akitoa elimu kwa Wananchi ndani ya Wilaya hiyo, "Tunapata malalamiko kutoka kwa Wananchi kuwa mnafanya matukio ya ajabu na ubabe kisa tu ninyi ni Polisi Jamii, hii sio sawa acheni kukamata Watu bila kufuata utaratibu mzuri , Biashara haramu na matendo mengine yanayokinzana na sheria za nchi ninyi muwe mfano hakuna aliye juu ya sheria."



No comments:

Post a Comment