Bondia wa ngumi za kulipwa nchini Amiri Rashid Matumla a.k.a 'Snake Boy Jr' ametangaza wazii kumtaka ndani ya ulingo bondia kutoka Mabibo King Of Naccoz Camp Mfaume Mfaume a.k.a 'Mapafu ya Mbwa'.
Amiri huyu ni mtoto pekee wa Mzee Rashid Ally Matumla Legendary wa mchezo wa Masumbwii hapa nyumbani anaecheza ngumi kijana huyo ameonyesha niya ya kumtaka bondia Mfaume ili kulipiza kisasi cha mchezo wa Ndondi kwa ndugu yake na kaka ake mkubwa Mohammed Matumla.
Itakumbukwa Mfaume na Mohammed waliwahii kukutana Tarehe 5/2/2017 kwenye pambano la utangulizi la raundi 8 lililowahii kupigwa Uwanja wa ndani wa Taifa na bondia Mohammed Matumla alipoteza pambano hilo kwa matokeo ya 'K.O' kwenye raundi ya 7 tukio ambalo lililomletea madhara na itilafuu kwenye kichwa chake na kusababisha yeye kuachana na mchezo wa Masumbwii.
Baada ya tukio hilo imepita miaka 7 sasa na kimevumbuliwa kipaji kingine kutoka kwenye familia hiyo ya Matumla familia ambayo ina historia nzuri na mchezo huu wa Masumbwii.
Na kwa mujibu wa mtandao wa Boxrec Amiri ni bondia kinara wa uzani wa Super Welterweight kg 69 hapa nyumbani akishika nafasi ya kwanza kati ya mabondia 26 wanaocheza uzani huo wa kg 69 hapa nyumbani akiwemo bondia Mfaume.
Ambae kwa sasa rekodi yake ipo Inactive kwenye upande wa nafasi kutokana nakuto kucheza kwa mda mrefu kidogo tangu alivyocheza pambano lake la mwisho mwaka jana dhidi ya bondia Chikondi Makawa raia wa Malawi na kuibuka mshindi kwa matokeo ya point ya majaji wote watatu.
Baada ya sakata hilo baadhii ya wadau wa mchezo wa Ndondi kila mmoja kwa nafasi yake wamekuwa wakitoa maoni yao tofauti tofauti kwenye sakata hilo kwani wapo wanao ona kijana ni wakati wake sahihi wa kucheza na bondia Mfaume Mfaume.
Na kuna wengine wamekuwa na maoni tofauti kwamba kijana huyo huu sii wakati mzuri kwa upande wake kucheza na bondia huyo anahitajika kukuwa na kukomaa kidogo kwa kucheza mapambano kadhaa magumu kabla ya kumvaa bondia Mfaume Mfaume.
Amiri ana Totally Fight's 5, Win's 5, 'KO'S' 2, Lose 0 & Draw 0.
Mfaume ana Totally Fight's 28, Win's 18, 'KO'S' 8, Lose 8 & Draw 2.
No comments:
Post a Comment