Hii ni blog ambayo inakupa Taarifa na habari Zote Za Kitaifa na za kimataifa Katika Nyanja Zote za kisiasa, Uchumi, michezo na burudani..

Tuesday, April 1, 2025

Kapteni Ibrahim Traore Rais na Kiongozi wa jeshi la Burkina Faso, ametoa msamaha kwa wanajeshi 21 waliohusika katika mapinduzi ya serikali ya Septemba 2015.


Katika amri iliyotiwa saini Machi 24 Kapteni Traore aliweka masharti ya msamaha, ambao ulipigiwa kura mnamo Desemba iliyopita na bunge la mpito.


Wanajeshi hao 21, wakiwemo maafisa, maafisa wasio na kamisheni na vyeo vingine, walifikishwa mahakamani au kutiwa hatiani kwa matendo yaliyofanywa Septemba 15 na 16, 2015, inasema amri iliyotiwa saini na Kapteni Ibrahim Traore.


Hata hivyo, amri hiyo inaeleza kuwa kurejeshwa kazini kufuatia msamaha hakuwezi kutoa mwanya wa urekebishaji wa kazi au fidia.


Kutiwa saini kwa amri hii kunafuatia kupitishwa mwishoni mwa Desemba 2024, na bunge la mpito, kwa sheria ya msamaha na masharti ya kutoa msamaha kwa watu waliopatikana na hatia kuhusiana na mapinduzi yaliyofeli ya 2015.



Sheria hii inabainisha kwamba askari waliotiwa hatiani au kufunguliwa mashtaka kuhusiana na kesi hii, na wanaoonyesha kujitolea katika mapambano dhidi ya ugaidi, wanaweza kuchukua fursa ya neema ya msamaha ili kupandishwa cheo katika kazi zao. 

No comments:

Post a Comment