Hii ni blog ambayo inakupa Taarifa na habari Zote Za Kitaifa na za kimataifa Katika Nyanja Zote za kisiasa, Uchumi, michezo na burudani..

Saturday, November 14, 2015

Francis Cheka mafichoni kumkabili Tomas Mashali





Bondia wa ngumi za kulipwa Tanzania Francis Cheka ameingia mafichoni kujiandaa kwa pambano lisilo la ubingwa la Round 12 dhidi ya Tomas Mashali, lililo pangwa kufanyika Desemba 25 mwaka huu, katika uwanja wa jamuhuri mjini Morogoro.
 
Bondia francis Cheka akipewa mafunzo na master wake.
Akizungumzia pambano hilo Cheka alisema kwa kuwa Tomas Mashali ametamba kuwa atampiga kasha atastaafu, yeye ameanza kujifua mapema ili aweze kumchapa katika round za mwanzo.


Alisema amepania kuweka historia mpya kwa kumtwanga mapema mpinzani wake na kukata ngebe zake, huku akieleza kuwa kitendo cha kutamba mpinzani wake kimemuongezea hasira, hivyo atamstaafisha kupigana ngumi mara baada ya kumuadhibu katika Round tatu za mwanzo.
Bondia Tomas Mashali.


 “yeye si anataka kuachana na masumbwi kwa kuweka historia ya kunipiga, basi nitaingia mafichoni kwa ajili yake na tutakapo kutana ajiandae kupata kipigo cha historia kutoka kwangu” alisema Cheka
Tomas Mashali (kushoto) akisaini mkataba dhidi ya pambano lake na Francis Cheka, katikati ni Promota wa ngumi Kaige Siraju.

Aidha alimaliza kwa kusema ataonyesha vitendo kwenye ulingo ili aweze kuongeza heshima ya katika medani ya ngumi.

No comments:

Post a Comment