Vifaa vya mchezo wa Judo vilivyotolewa na Shirikisho la
mchezo huo Duniani IJF, viko hatarini kupigwa mnada baada ya chama cha Judo
Tanzania JATA, kushindwa kulipia ushuru
ili kuvigomboa bandarini.
Akizungumziasakata hilo Katibu mkuu wa JATA, Innocent Malya
amesema chama chake kimeshindwa kulipa ushuru ili kuvikomboa vifaa hivyo
kutokana na changamoto mbalimbali na hivyo huenda vikapigwa mnada.
Malya alisema wakiamua kuwaambia ukweli JIF, kwamba
wameshindwa kulipia ushuru ili vifaa virudishwa viliko toka huenda waka vipeleka na hicho ndicho kikwazo
kingine baada ya selikari kutaka vilipiwe deni wanalo daiwa ambapo IJF,
ilisaidia kwa kutoa sh. milioni 3.6, na kilicho baki kilikuwa sh. milioni 9.2
ili viweze kutolewa.
![]() |
Baadhi ya wanafunzi wa JUDO nchini Tanzania wakionyesha bendera ya Taifa. |
Hata hivyom alisema kinacho elekea kutokea kinafanana na
kilichowahi kufanyika mwaka 2006, ambapo JIF iltoa vifaa lakini vilikwama
bandalini baada ya kukosekana kwa fedha za kulipia ushuru hatua iliyom
sababisha vipigwe mnada.
No comments:
Post a Comment